• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaendeleza ubabe UMITASHUMTA

Posted on: August 10th, 2022

MARA YAENDELEZA UBABE UMITASHUMTA

Mkoa wa Mara umeendeleza ushindi katika Mashindano ya 26 ya Umoja wa Michezo na Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) mwaka 2022 baada ya kuibuka mshindi wa pili wa jumla kwa kupata pointi 125.2.

Akizungumza baada ya kupokea matokeo hayo, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Bwana Benjamin Oganga ameeleza kuwa katika mashindano hayo, Mkoa wa Mara umefanikiwa kushinda jumla ya makombe manne.

Bwana Oganga ameeleza kuwa mikoa mingine iliyofanya vizuri katika UMITASHUMTA ni Mwanza ambao umeongoza kitaifa kwa kupata pointi 160.3; na kufuatiwa na Mkoa wa Mara wenye pointi 125.2, Mkoa wa Tabora wenye pointi 115.7, Mkoa wa Geita (109.7) na Mkoa wa Dar es Salaam ambao umepata jumla ya pointi (109.5).

Bwana Oganga ameeleza kuwa katika mashindano hayo Mikoa ambayo haikufanya vizuri sana ni pamoja na Unguja yenye pointi 24.2, Pemba yenye pointi 28.4, Mkoa wa Ruvuma wenye pointi 39.7 na Mkoa wa Katavi ambao umepata pointi 45.9.

Bwana Oganga ameeleza kuwa katika mashindano hayo, Mkoa wa Mara umefanya vizuri katika  Nidhamu na Usafi ambapo kwa wasichana wamekuwa washindi wa kwanza wakati kwa wavulana wamekuwa washindi wapili.  

Mashindano ya UMITASHUMTA ilifunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Dkt. Charles Msonde na kufungwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Pauline Gekul.

Akifunga mashindano hayo katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora, Mheshimiwa Gekul ameitaka Mikoa na Halmashauri zote nchini kusimamia ushiriki wa shule za binafsi katika mashindano ya michezo kwa wanafunzi.

Mwaka 2021 Mkoa wa Mara ulikuwa mshindi wa kwanza wa UMITASHUMTA Kitaifa nafasi ambayo imechukuliwa na Mkoa wa Mwanza kwa mwaka 2022.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa