• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yaazimia kuboresha ufaulu wa wanafunzi

Posted on: July 14th, 2021

Mkoa wa Mara umeazimia kuboresha ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya taifa ya kumaliza Elimu ya Msingi na mtihani wa Kidato cha Nne kwa mwaka 2021.

Hayo yameelezwa leo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela wakati akizungumza katika kikao cha wasimamizi wa elimu Mkoa wa Mara cha kutangaza matokeo ya mtihani wa utimilifu (Mock) kwa Kidato cha Nne kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji.

“Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Hapi ameagiza kuwa wataalamu wa elimu na wote wanaohusika na mitihani wafanye maandalizi yote kwa ajili ya mtihani hiyo na kuhakikisha kuwa Mkoa unashika nafasi nzuri kitaifa” alisema Bwana Msovela.

Bwana Msovela ameeleza kuwa Mheshimiwa Hapi ametaka Mkoa kushika angalau nafasi ya kumi katika mtihani wa kidato cha nne na mtihani wa kumaliza elimu ya msingi.

Aidha amewataka wakurugenzi wa Halmashauri kuangalia uwezekano wa kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi hasa walio katika madarasa ya mitihani ili kuwapunguzia muda wa kutafuta chakula na badala yake watumie muda huo katika maandalizi ya mtihani.

Bwana Msovela ameahidi kuzitembelea shule zote zilizofanya vibaya katika mtihani huo ili kuangalia kinachowakwamisha wanafunzi wao kufanya vizuri katika mtihani.

Akizungumza katika mkutano huo, Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara Bwana Benjamin Odunga ameeleza kuwa mtihani wa utimilifu kwa wanafunzi wa kidato cha nne kwa Mkoa wa Mara ulifanyika kuanzia tarehe 02 Juni 2021 hadi tarehe 18 Juni 2021 ukiwa na lengo la kupima matayarisho ya wanafunzi kwa ajili ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka 2021. 

Akisoma matokeo ya ufaulu wa mtihani huo, Bwana Odunga ameeleza kuwa wanafunzi wamefaulu kwa wastani wa asilimia 78.26 na kuongeza kuwa kwa mwaka huu ufaulu umepanda kwa asilimia 9.47 ukilinganisha na mtihani kama huo wa mwaka 2020 ambapo mkoa ulikuwa na ufaulu wa asilimia 68.79.

Bwana Odunga amewataja wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika mtihani huo kuwa ni Irene Thomas Wegesa (Twibhoki), Dorcas Julius Simon (Kowak Girls), Kelly Daniel Chacha (Twibhoki), Emannuel Mrema Emmanuel (Musoma Technical), Jackline Werema Audax (Twibhoki), Paulo Joseph Gidamariri (Musoma Technical), Julius Abel Maginga (Angel House) na Irene Charles Balele (Kowak Girls).

Aidha amezitaja shule zilizofanya vizuri zaidi katika mitihani hiyo kuwa ni Twibhoki (Serengeti), Kitenga Girls (Tarime), Kowak Girls (Rorya), Chief Wanzagi (Butiama), Angel House (Tarime),Girango (Rorya), Dr. John Chacha (Tarime), Makoko Seminary na Amani (Musoma) na Mahende ya mji wa Bunda.

Bwana Odunga amezitaja halmashauri zilizofanya vizuri katika mtihani huo kuwa ni Halmashauri ya Mji wa Bunda ikifuatiwa na Manispaa ya Musoma, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Halmashauri nyingine kulingana na matokeo hayo ni Halmashauri ya Mji wa Tarime, Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ambayo ilikuwa ya mwisho kwa ufaulu.

Mwalimu Oganga ameeleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa kupata daraja la kwanza hadi la tatu ni asilimia 23.85 tu ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo na wanafunzi wengine wote waliobakia wamefeli.

“Wanafunzi waliopata daraja sifuri ni 4,874 wakati wanafunzi waliopata daraja la nne ni 12,203. Jumla ya wanafunzi waliopata daraja la nne na sifuri ni wanafunzi 16,077 ambapo ni sawa na asilimia 76.15 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani” ameeleza Bwana Oganga.  

Bwana Oganga ameeleza kuwa Mkoa umejiwekea lengo la ufaulu wa asilimia 95 kwa mwaka 2021 katika mtihani huo na kufaulisha kwa asilimia 100 katika mtihani wa taifa ambapo kwa daraja la kwanza hadi la tatu kuwa na ufaulu wa asilimia 50 wakati daraja la nne kufikia asilimia 50. 

Bwana Oganga ameeleza kuwa jumla ya masomo 24 yalitahiniwa katika mtihani huo na asilimia 5.34 tu ya watahiniwa wote wamefaulu katika somo la Hisabati huku Kiswahili kikiongoza kwa kufaulisha asilimia 80.91 ya watahiniwa wote.

Bwana Oganga ameeleza kuwa matokeo hayo hayaridhishi ukilinganisha na malengo ya Mkoa na hata ya kitaifa hivyo mkoa unahitaji kuongeza nguvu ya pamoja katika ufuatiliaji wa ufundishaji na ujifunzaji ikiwa ni pamoja na kuwatia moyo walimu.

Katika kikao hicho maazimio mbalimbali yalifikiwa ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi ikiwa ni pamoja na kutembelea shule zilizofanya vibaya, kutoa chakula shuleni kwa wanafunzi wa madarasa ya mitihani, kuwatumia walimu wenye umahiri katika baadhi ya masomo ili kuwasaidia wanafunzi na kuendelea kufuatilia ufundishaji wa walimu pamoja na mambo mengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa