• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima: Uchunguzi Unaendelea

Posted on: April 13th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amezungumzia maendeleo ya uchunguzi uliokuwa unafanyika kuhusiana na watu waliohisiwa kukwama chini ya Mgodi wa North Mara walipoingia humo kwa nia ya kuiba.  

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 9 Aprili 2021 Mheshimiwa Malima amesema kuwa kwa sasa hamna watu waliokwama chini ya mgodi lakini uchunguzi unaonyesha kuwa kulikuwa na watu walioingia na kutoka chini ya mgodi huo.  

“Kwa sasa vyombo vya dola vinahitaji kuwahoji watuhumiwa watano ambao walikuwa wanajihusisha na kufadhili makundi ya vijana waliokuwa wanakwenda kuiba ndani ya Mgodi wa North Mara kwa mahojiano zaidi” alisema Mheshimiwa Malima.

Amewataja watuhumiwa kuwa ni Bwana Rafael Matiku Zakaria ambaye ni mfanyabiashara katika eneo la Bweri, Manispaa ya Musoma; Bwana Keraha Yohana Shona ambaye ni mfanyabiashara katika eneo la Nyamongo wilayani Tarime na Bwana Manase Kazota Philemon mkazi wa Buswelu mkoani Mwanza.

Watuhumiwa wengine ni wanaohitajika katika ukamilishaji wa uchunguzi huo ni Bwana Makenge Chacha Nyaisa mkazi wa Nyamwaga, Tarime na Bwana Nyagwisi Charles Marwa Mkazi wa Tarime.

“Watuhumiwa wote hawa wanatakiwa kujisalimisha katika ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara au Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Tarime/Rorya haraka iwezekanavyo kabla jeshi halijaanza kuwatafuta” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kwa pamoja wamekuwa wakifadhili baadhi ya vijana kuingia katika Mgodi wa North Mara unaomilikiwa kiubia kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya Barrick.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Malima ameongelea kuhusiana na maendeleo ya uchunguzi wa udanganyifu uliofanyika katika malipo ya fidia kwa wananchi wa vijiji viwili katika eneo la Nyamongo.

“Uchunguzi umefikia katika hatua nzuri na kwa sasa watuhumiwa 16 wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili” alisema Malima.

Ameeleza kuwa mpaka sasa uchunguzi umebaini katika ya fedha zote zaidi ya bilioni 30 zilizolipwa fidia, zaidi ya bilioni mbili zililipwa kwa watu waliotoa vielelezo visivyo sahihi na hivyo hawastahili malipo hayo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa