• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima: Toeni Elimu ya Uchaguzi

Posted on: August 24th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima ameitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa kutoa elimu zaidi kuhusiana na masuala muhimu ya uchaguzi kwa wasimamizi na wadau wa uchaguzi ili kuimarisha demokrasia hapa nchini.

Mheshimiwa Malima amesema hayo leo tarehe 24 Agosti 2020 ofisini kwake wakati alipowapokea maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Kanda ya Ziwa Mashariki ambao watasimamia uchaguzi katika Mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga.

“Wasimamizi wa uchaguzi kwa ngazi zote wanahitaji elimu ya sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kuimarisha demokrasia yetu hapa Tanzania”. Alisema Mheshimiwa Malima.

Ameeleza kuwa elimu juu ya sheria hizi katika ngazi mbalimbali za usimamizi wa uchaguzi itaongeza uwajibikaji na kuimarisha picha ya demokrasia ya Tanzania kwa wadau wote ambao wangependa kuufuatilia.  

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kuna baadhi ya vyama vinajua kabisa havitashinda lakini vitajitahidi kuwekeza katika kuleta chokochoko ili kuvuruga uchaguzi na kuionyesha dunia kuwa uchaguzi wa Tanzania haukuwa wa haki.

Aidha Mheshimiwa Malima amemwagiza Mratibu wa Masuala ya Uchaguzi katika Mkoa wa Mara Bwana Dominick Rusasi kuandaa mafunzo ya sheria za vyama vya siasa na gharama za uchaguzi kwa Makatibu Tarafa na Watendaji wa Kata wa Mkoa wa Mara ili kuimarisha usimamizi wa uchaguzi.

Awali, maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyamavya siasa waliotoa pendekezo la kutoa mafunzo kuhusiana na sheria hizo kwa wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya majimbo na wasimamizi wa uchaguzi kwa ngazi ya Mkoa.

Maafisa waliojitambulisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara ni Bibi Clevu Sepaku, Msimamizi wa Uchaguzi Kanda ya Ziwa Mashariki ambaye aliambatana na Bwana Mtibora Suleiman na Bwana Frank Shija.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa