• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Malima awataka wananchi kuwasilisha malalamiko

Posted on: February 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amewataka wananchi na wadau mbalimbali wa mahakama kuwasilisha malalamiko yanayohusu maadili ya maafisa wa mahakama kwenye kamati ya Mkoa ya kushughulikia malalamiko hayo ili yaweze kufanyiwa kazi kwa mujibu ya sheria.

Mheshimiwa Malima ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Februari 2021 wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na masuala mbalimbali ya maendeleo kwa Mkoa wa Mara.

“Natoa wito kwa wananchi wote wenye malalamiko yanayohusu maadili ya maafisa wa mahakama kuwasilisha malalamiko yao kwa maandishi na kamati yangu itatenda haki ya kusikiliza pande zote mbili zinazohusika kabla ya kutoa mapendekezo kwa Jaji Mfawidhi” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 50 cha Sheria ya Utumishi wa Mahakama Namba 4 ya mwaka 2011 kamati ya maadili inaongozwa na yeye kama mwenyekiti wake na wajumbe wengine sita ambao ni pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa ambaye ndiye kaatibu wa kamati hiyo.

Ameeleza kuwa majukumu ya kamati ya maadili wa maafisa wa mahakama ni kuchunguza malalamiko ya ukiukwaji wa maadili dhidi ya mahakimu na wasaidizi wa sheria wa majaji na kufanya maamuzi na kuandaa repoti ya uchunguzi wa malalamiko.   

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima wananchi wanaweza kulalamikia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na namna kesi ilivyoshughulikiwa; tuhuma za rushwa; kushindwa kutekeleza majukumu na vitendo vinavyokiuka kanuni za maadili ya maafisa wa mahakama.

Aidha amewataka wananchi kutoa malalamiko yao kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ndani ya miezi sita baada ya tukio kutokea kwa maandishi na kwa lugha ya Kiswahili ili kamati iweze kuyafanyia kazi malalamiko yao.

Mheshimiwa Malima ameahidi kamati hiyo kutenda haki katika kusikiliza na kushughulikia malalamiko yatakayowasilishwa kabla ya kutoa mapendekezo ya kamati kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa