• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Makungu ataka mabadiliko sekta ya afya

Posted on: January 27th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amefanya kikao na wasimamizi wa afya katika Halmashauri na Wakuu wa Vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara na kuwataka kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya.

Akizungumza katika kikao hicho Bwana Makungu ameeleza matamanio yake kuwa Mkoa wa Mara uwe Mkoa wa mfano katika utoaji wa huduma bora za afya na mikoa mingine waje kuiga Mara.  

“Sisi tuwe Mkoa ambao unatoa huduma bora za afya, huduma nzuri na kwa wakati, lugha nzuri kwa wagonjwa, tufanye kazi kama timu moja ili kuondoa changamoto mbalimbali zinazotukabili na kujenga uhusiano mzuri katika maeneo yetu ya kazi, tutafanikiwa” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu amewataka wasimamizi na wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Mara kutimiza wajibu wao ili kuwa wa mfano kwa watumishi waliochini yao na kuhakikisha vituo vya kutolea huduma za afya havigeuki kuwa vituo vya malalamiko ya wananchi.

Aidha, Bwana Makungu amewahimiza watumishi woe wa sekta ya afya kuisaidia Serikali katika kutekeleza sheria ya mtoto ambayo inapiga marufuku vitendo vya ukeketaji katika jamii ili kuwanusuru watoto wakike kutokana na ukeketaji.

Bwana Makungu amewahimiza watumishi kuzijua sheria za utumishi wa umma ili kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Katibu Tawala amewahimiza wasimamizi wa sekta ya afya na wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya kutoa elimu kwa wananchi wote kuhusiana na umuhimu wa Bima ya Afya ili wananchi waweze kujiunga na kupata huduma za afya kwa urahisi zaidi.

Wakati huo huo, Bwana Makungu amewataka wasimamizi wa sekta ya afya kuhakikisha mifumo ya kukusanya mapato katika vituo vya kutolea huduma za afya inafungwa sehemu zote muhimu na inafanyakazi ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Zabron Masatu amemshukuru Katibu Tawala kwa kutenga muda wake kuzungumza na wasimamizi wa sekta ya afya na kuahidi kuyafuatilia mambo yote yaliyozungumzwa katika kikao hicho.

Akizungumza kuhusiana na rasimu ya Mfuko ya Bima ya Afya kwa wote, Dkt. Masatu amesema mfuko huu utakuwa ni mkombozi wa watanzania walio wengi katika kupata huduma za afya za uhakika wakati wote wanapohitaji.

Dkt. Masatu amewataka wasimamizi wa afya katika Halmashauri kutoa elimu kuhusu mpango wa serikali kwa wananchi ili waweze kuelewa na kuchukua hatua za kuunga mkono juhudi za serikali kuboresha huduma za afya.

Katika kikao hicho pia watumishi walipata nafasi ya kusikilisha wasilisho la Shiria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma na rushwa katika mazingira ya kazi.

Matangazo ya Kawaida

  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 MKOA WA MARA December 18, 2020
  • NAFASI ZA KAZI KWA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI, HISABATI, FUNDI SANIFU MAABARA NA LUGHA June 21, 2018
  • Mara yapaa Kimichezo July 20, 2019
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP April 23, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mpango wa M-Mama watambulishwa Mara

    February 16, 2023
  • RC aitaka RUWASA kutoa taarifa ya vyanzo vya maji

    February 10, 2023
  • Nyanungu watakiwa kuitumia fursa vizuri

    February 10, 2023
  • RC avitaka vyama vya watu wenye ulemavu kuanzisha miradi

    February 10, 2023
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: P.o.Box 299 Musoma

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa