• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kiongozi wa Mbio za Mwenge akipongeza kikundi cha bodaboda Rorya

Posted on: June 24th, 2021

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AKIPONGEZA KIKUNDI CHA BODABODA RORYA

Kiongozi wa Kitaifa wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Maalum Lt. Josephine Paul Mwambashi amekipongeza kikundi cha bodaboda cha vijana kutokana na uaminifu wao katika kurudisha mkopo waliopewa na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Bibi Mwambashi ametoa pongezi hizo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikundi hicho na kuelezea kufurahishwa kwake kwa namna vijana hao walivyojenga uaminifu na sasa kwa kutumia uaminifu huo wamekopeshwa tena.

“Nataka niwapongeze kwa uaminifu wenu mlioufanya katika biashara zenu na kufanikiwa kurejesha mkopo wa halmashauri kwa wakati na hivyo mkafanikiwa kupata mkopo mwingine tena” alisema Mwambashi.

Hata hivyo aliwataka vijana hao kuzingatia sheria za barabarani wakati wakiendesha pikipiki hizo kwa usalama wa maisha yao na wananchi wengine.

“Kumekuwa na ajari nyingi za pikipiki na kuhatarisha maisha ya madereva, watumiaji wa pikipiki na wakati mwingine hata watumiaji wengine wa barabara kutokana na kutokuzingatia sheria za usalama wa barabarani” alisema Mwambashi.  

Hata hivyo Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Rorya kuhifadhi pikipiki moja mpaka wanaopatiwa mafunzo wafuzu na waje na lesseni ya udereva.

Awali akisoma taarifa ya kikundi hicho Mwenyekiti wa Kikundi hicho Bwana James Msigwa ameeleza kuwa kikundi hicho kilipewa mkopo na Halmashauri ya Wilaya ya Rorya wa shilingi milioni tano ambazo walitumia kununua pikipiki mbili na kuanzisha biashara yao.

“Ule mkopo tulipomaliza kuurejesha ndani ya muda tuliyokuwa tumepangiwa, tukapatiwa tena mkopo mwingine wa kununua pikipiki nyingine mbili ili kupanua mradi wetu.

Bwana Msigwa amesema kuwa kikundi  hicho ni cha vijana kumi ambao waliamua kujiunga pamoja na kuanzisha biashara yao.

Kati ya vijana hao vijana watatu wanaleseni za udereva, kijana mmoja analeseni iliyoisha muda wake wa matumizi na vijana wengine sita wapo katika mafunzo ya udereva.

Wakati huo huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa amelipongeza Jeshi la Polisi kwa jitihada kubwa linafanya katika kukamata madawa ya kulevya.

Hata hivyo amekataa kuteketeza bangi zilizokamatwa katika Wilaya ya Rorya kutokana na eneo hilo kuwa karibu na makazi ya watu.

Mwenge wa Uhuru leo umeendelea na mbio zake katika Wilaya ya Rorya ambapo umepokelewa katika eneo la Nyanchabakenye kutoka Wilaya ya Tarime na unatarajiwa kukabidhiwa kesho kwa Wilaya ya Musoma katika viwanja vya Mukendo vilivyopo katika Manispaa ya Musoma.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa