• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

Posted on: May 8th, 2025

Wananchi wa Wilaya ya Musoma Mkoani Mara wameendelea kuitikia wito wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Alfred Mtambi, kwa kuondoa uhaba madawati mashuleni na kutengeneza kwa hiari yao na kuyakabidhi kwa Serikali madawati kadhaa ambapo Mei 6, 2025 zimepokelwa pea mia moja za meza na viti kutoka Jumuiya ya Waisilamu wa Manispaa ya Musoma.

Akipokea msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuliwekea msistizo suala la madawati kwa wanafunzi wa Mkoa wa Mara na hivyo kuwa suluhu ya changamoto ya madawati kwa wanafunzi.

“Mkuu wa Mkoa wa Mara amekuwa anasisitiza kuwepo mahusiano bora baina ya Serikali na taasisi zilizopo katika Mkoa zikiwamo taasisi za dini. Hongereni sana kwa kufanya jambo hili. Mkuu wa Mkoa amenielekeza nipokee madawati haya na anatoa asante sana” amesema Mhe. Chikoka.

Akizungumza katika hafla hii fupi mbele ya Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mara Shehe wa Mkoa wa Mara Ustadh Kassimu Msabaha amempongeza Mkuu wa Mkoa Mara kwa kushirikiana nao katika kila jambo analohusishwa.

Shehe Msabaha amesema Mhe. Mtambi anafanya mambo menngi mazuri ya kuileta jamii pamoja na kuongeza kuwa hilo ni jambo zuri na huo ndiyo utamaduni wa Watanzania.

Katika hafla hiyo risala ya makabidhiano iliyosomwa na Ustadhi Rashid Saad Kaema ilinadi kuwa “Sambamba na pea hizo 100 za meza na viti, Jumuiya ya Waisilamu  Manispaa ya Musoma tutaendelea kushirikiana na Serikali zaidi na zaidi na kadili na majaliwa na Mwenyenzi Mungu.”

Akishukuru kwa Niaba ya Halmshauri ya Wilaya ya Musoma, Afisa Elimu Taaluma Bi Easter Kakulima amesema “tuna upungufu wa madawati 3548 na kwa msaada huu tuliopokea Jumuiya ya Waislamu wa Musoma wametuunga mkono na tunawashukuru sana, Mungu awabariki.”

Mara baada ya makabidhiano haya lilifanyika dua la kuiombea nchi ya Tanzania, kumuombea Rais Samia na kuuombea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na dua hii imeongozwa na Shehe wa Mkoa wa Mara Ustadh Kassimu Msabaha.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa