• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

Posted on: May 20th, 2025

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara leo imeanza ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 katika Mkoa wa Mara na kuipongeza Serikali kwa utekelezaji mzuri wa ilani hiyo.

Akizungumza katika ziara ya kamati hiyo Wilaya ya Rorya, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Mhe. Patrick Chandi Marwa amesema miradi ya maendeleo yote aliyoikagua imetekelezwa vizuri na value for money katika miradi hiyo inaonekana.

“Mimi nimeridhika na utekelezaji wa miradi hii na ninaipongeza Serikali na watekelezaji na wasimamizi wa miradi kwa namna walivyotekeleza miradi hii katika Wilaya ya Rorya na kama Chama tumeridhika” amesema Mhe. Chandi Marwa.

Mhe. Chandi Marwa amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, viongozi wa ngazi ya Mkoa na Wilaya na watendaji wa Serikali kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo yenye tija ambayo inakisaidia Chama kuaminika kwa wananchi.

Mhe. Chandi Marwa amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Mara kufuatilia upelekaji wa huduma za umeme na maji katika miradi ya VETA na Shule ya Sekondari ya Jaffari Chege inayoendelea kujengwa ili kuwepo na huduma hizo wakati zitakapoanza kutoa mafunzo kwa wanafunzi.

Katika mradi wamiundombinu ya kilimo cha umwagiliaji Labour, Mhe. Chandi ameitaka Serikali kumsimamia mkandarasi kukamilisha mradi huo kwa haraka ili wananchi waweze kufaidika na mradi huo kwa kulima kilimo cha uhakika na kudhibiti ng’ombe wanaoingia katika maeneo hayo ili kulinda miundombinu iliyowekwa.

Akiwa katika mradi wa Maji Nyamunga, Mhe. Chandi pia amewasalimia wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Nyamunga na kutoa shilingi 500,000 kwa ajili ya kununua vifaa vya michezo baada ya wanafunzi kumwambia uwepo wa hitaji la vifaa vya michezo.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Meja Edward Gowelle amekipongeza Chama cha Mapinduzi kwa kutenga muda wa kukagua miradi inayotekelezwa na Serikali na kuwakaribisha viongozi wa CCM kukagua na kutoa maoni na maelekezo ya namna bora ya kutekeleza miradi hiyo.

“Sisi tunakipongeza sana Chama cha Mapinduzi kwa kupata muda wa kukagua miradi inayotekelezwa na Serikali yake na tupo tayari kupokea maoni na maelekezo kuhusiana na utekelezaji wa miradi hii” amesema Mhe. Gowelle.

Katika Wilaya ya Rorya Kamati ya Siasa ya Mkoa imekagua ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA Rorya, mradi wa maji ya bomba Nyamunga, ujenzi wa Shule ya Sekondari Jaffari Chege na mradi wa kilimo cha umwagiliaji Labour na kesho inaendelea katika Wilaya ya Tarime.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa ambao wamejigawa katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza limeongozwa na Mhe. Chandi Marwa, kundi la pili limeongozwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Mara Mhe. Iddi Mkoa huku kundi la tatu limeongozwa na Mjumbe wa NEC Mhe. Christopher Gachuma na kufanya ukaguzi katika Wilaya za Rorya, Serengeti na Musoma.

Kesho tarehe 21 Mei, 2025 Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mara itahitimisha ukaguzi wake kwa kutembelea miradi katika Wilaya za Tarime, Bunda na Butiama.

Kwa upande wa Rorya, ziara hiyo imehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Rorya, baadhi ya Watendaji wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara, Mwenyekiti, Mkurugenzi Mtendaji na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Rorya na wasimamizi wa miradi iliyotembelewa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa