• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Misaada ya maafa musoma kuwafikia walengwa

Posted on: April 17th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi leo tarehe 17 Aprili, 2025 amepokea msaada kutoka Mgodi wa Dhahabu wa North Mara na wazabuni wake kwa ajili ya waathirika waliokumbwa na maafa katika kata 10 za Manispaa ya Musoma na kuahidi kuwa Mkoa utasimamia misaada hiyo iweze kuwafikia walengwa waliokusudiwa.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mhe. Mtambi ameushukuru mgodi kwa kutoa shilingi 45, 240,000, mifuko 200 ya simenti na magodoro 20 na kuwahakikishia kuwa msaada huo utatumika kulingana na malengo yaliyokusudiwa.   

“Msaada huu umefika wakati muafaka ambapo tunaendelea kurejesha hali ya wananchi walioathirika katika maafa hayo kuwa nzuri zaidi kuliko hali waliokuwa nayo awali kabla ya maafa hayo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema kwa sasa baadhi ya wahanga wa maafa hao wamesaidiwa kuanza kuishi maisha yao ya kawaida katika maeneo waliyotoka na wale waliokuwa wapangaji wamesaidiwa kwa kulipiwa kodi ya miezi sita kulingana na kodi zao za awali.

“Baada ya msaada uliotolewa na Rais Samia, waathirika wengi wamerejea katika hali zao za awali, aidha familia tatu ambazo nyumba zao ziliathirika zaidi zimejengewa nyumba mpya na kupatiwa majiko yanayotumia nishati safi ya kupikia” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema bado kuna watu wanaohitaji msaada ikiwemo ukarabati mkubwa wa nyumba zao ili waweze kurejea katika hali yao ya awali na ikiwezekana wapate hali bora zaidi.

Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuzipongeza Kamati ya Usalama na Kamati ya Maafa Mkoa na Wilaya ya Musoma kwa kazi nzuri walizofanya katika utekelezaji wa zoezi la kuwahudumia wahanga wa maafa hayo na kufanikisha kurejesha hali zao za awali kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amesema katika maafa hayo jumla ya kata 10 ziliathirika na kaya 319 zenye watu 1,227 ziliathirika na maafa hayo ikiwa ni pamoja na majengo ya taasisi za Serikali, biashara na dini.

Mhe. Chikoka ameushukuru Mgodi wa North Mara kwa kusaidia jitihada za Serikali za kuwarejesha wahanga wa maafa hayo katika hali nzuri ili waendelee kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kwa upande wake Meneja Mahusiano wa Mgodi wa Dhahabu North Mara Bwana Francis Uhadi amesema Mgodi wa Dhahabu wa North Mara kwa kushirikiana na wazabuni mbalimbali waliopo mgodini hapo umetoa msaada wa fedha taslimu na vifaa.

Bwana Uhadi amesema Mgodi unatoa msaada wa fedha tasilimu shilingi 45,240,000 na tani kumi za simenti na magodoro 20 kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa maafa hayo.

Bwana Uhadi amesema Mgodi unatoa pole nyingi kwa wote waliofikwa na maafa hayo pamoja na viongozi na watumishi wa Serikali ambao walishiriki kwa namna moja au nyingine kutoa msaada wa kibinadamu kwa waathirika hao.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa