• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yapaa Kimichezo

20 July 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema kuwa pamoja na Mkoa wake kufanya vibaya katika matokeo ya mtihani wa kitaifa kidato cha sita mwaka huu lakini bado kuna fursa ya kufanya vizuri zaidi katika mitihani ijayo ya kitaifa.

Akipokea vikombe vya ushindi kwa michezo ambayo timu za Mkoa wa Mara zilipata kwenye mashindano ya Umisseta na Umitashumita mwaka huu, Malima amesema kuwa Mkoa  bado una nafasi ya kufanya vizuri endapo kila mmoja wetu atatimiza majukumu na wajibu wake kama inavyotakiwa. Ni lazima mikakati, ufuatiliaji na usimamizi wa nidhamu kwa walimu na wanafunzi vifanyike kwa ukaribu zaidi ili kuweza kupiga hatua kutoka hapa tulipo , alisema Malima.

Aidha ,Malima aliwataka walimu Mkoani Mara kujipanga vizuri ili kuhakikisha kuwa Mkoa unafanya vizuri kitaaluma kwa manufaa ya watoto wa Mkoa wa Mara na taifa kwa ujumla. “Haiwezekani tuwe tunafanya vizuri katika Michezo lakini kwenye taaluma tunashika mikia. Ni lazima Mkoa ujipange ili jitihada zilizotumika katika kuhakikisha Mkoa unafanya vizuri kwenye michezo ya Umisseta na Umitashumita iliyofanyika kitaifa Mkoani Mtwara na kupelekea Mkoa wa Mara kuwa mshindi wa tatu kitaifa zitumike pia katika kuhakikisha kuwa Mkoa unafanya vizuri kitaaluma na kupandisha ufaulu katika mitihani ya kitaifa kuanzia ngazi ya msingi hadi sekondari.”alisisitiza Malima.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Afisa elimu wa Mkoa wa Mara Bw. Emmanuel Kisongo amesema licha ya kufanya vizuri katika Michezo ,Mkoa umeweka mikakati kabambe ya kuhakikisha ufaulu unapanda  kwenye mitihani ijayo ya kitaifa.

“Ni kweli kuwa hatujafanya vizuri kwenye taaluma kama Mkoa  na hilo halina ubishi ,lakini tunajipanga na kuendelea kusisitizana kila mmoja wetu awajibike anapostahili ili tutokane na aibu hii.”alisema Kisongo.

Mkoa wa Mara ni Mkoa mkongwe ambapo muasisi wa taifa hili Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere alizaliwa.Ni moja ya Mikoa iliyoka kanda ya ziwa.

Imeandaliwa na 

Stephano Amoni

Afisa Habari –Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa